WAZEE WILAYANI LUDEWA WATAKIWA KUJIKITA KATIKA KILIMO CHA MBOGAMBOGA NA MITI.


Shamba jipya la migomba na Mboga la mzee Aidan Ngailo Wipata


Shamba la miti la mzee Aidan Ngailo Wipata
Mzee Aidan Ngailo Wipata akiwa shambani kwake


Shamba la mboga
Shamba la miti


Wazee wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wametakiwa kujikita katika kilimo cha mbogamboga na upandaji wa miti badala ya kukaa na kucheza bao pia kushida katika vilabu vya pombe za kienyeji ili kujikwamua kiuchumi na kuacha dhana ya utegemezi ya kusubiri misaada kutoka kwa watoto na wajukuu wao wanaoishi mijini.

Hayo yamesemwa jana na Mzee Aidan Ngailo alimaalufu kwa jina la Wipata shambani kwake kitongoji cha Kibito kijiji cha Madindo kata ya Ludende wilayani Ludewa alipotembelewa na waandishi wa Habari ili kujionea mafanikio ya maze huyo mwenye umri wa miaka 68 ambaye amekuwa maalufu kutokana na shughuri zake za kilimo.

Mzee Wipata alisema kuwa Idadi kubwa ya wazee wamekuwa ni watu wa kulalamika na kuwasubiri watoto wao wawasaidie kwa kila jambo wakati uwezo wa kuanzisha kilimo cha mboga mbaga na matunda pia upandaji wa miti wanao lakini huishia kushinda kucheza bao na kulewa pombe za asili vilabuni,hali hiyo sio sahihi kwani kama kila mzee ataamua kujishughurisha hata vijana wazembe wataiga mfano huo.

Alisema kuwa awali wakatia anaanza kilimo hicho baada ya kuacha na na kilimo cha mahindi pia kufunga hoteli yake iliyokuwa Ludewa Mjini wazee wenzie walimcheka na kumuona kafilisika kwani aliuhama mji na kuhamia mashambani huku nyumba zake zote akizipangisha,lakini kwa sasa anamiliki zaidi ya Hekali miatatu za miti wakati migomba pekee kunahekali ishilini pia mboga za majani anahekali tano.

“Mboga na miti pamoja na kilimo cha migomba nimekuwa nikivuna fedha nyingi tofauti na nilipokuwa ninaishi Ludewa mjini,hivi sasa kwa mwaka ninauhakika wa kuingiza zaidi ya milioni themanini hivyo sina shida katika uendeshaji wa maisha yangu hata wazee wenzangu niliowaacha mjini muda mwingi wakivaa tai wameanza kuniomba ushauri kwa kuona nimefanikiwa licha ya kuwa umri umekwenda”,alisema maze Wipata.

Alisema kuwa alipofika katika kitongoji cha kibito alianza kwa kununua ekali tisa na kunaza kilimo cha mboga na migomba mwaka 2011 lakini mpaka sasa anamiliki zaidi ya ekali miatatu na tayari ameshazikatia hati miliki hivyo kuifanya Ardhi hiyo iweze kukopesheka kiurahisi tofauti na ilivyokuwa awali.

Mzee Wipata alisema kuwa vijana na wazee wengine baada ya kuona kuwa ananufaika na kilimo pamoja na upandaji miti wameanza kuhangaika kutafuta mashamba wakati wameshachelewa maeneo makubwa na yenye Rutuba wajanja kama yeye wameshayawahi na tayari yanamilikiwa kisheria hivyo amewataka wananchi wengine wanaotaka kuwa kama yeye kuchangamkia maeneo katika vijiji vingine vyenye rotuba.

Mwisho.



Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: