RONALDO SASA NDIO MCHEZAJI TAJIRI ZAIDI DUNIANI

Chris Brunskill Ltd/Getty Images 
NYOTA wa Real Madrid na Ureno, Cristiano Ronaldo sasa ni kati ya wanamichezo wanne wanaoongoza kwa kuingiza fedha duniani, wakizidiwa tu mwanamuziki Taylor Swift, Boyband One Direction na James Patterson.
Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa za jarida la Forbes ambalo limesema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 anaingiza kiasi cha dola za Kimarekani Milioni 88 kwa msimu. 
Kiasi hicho kinamuweka juu ya mpinzani wake mkubwa, Lionel Messi wa Barcelona anayeingiza dola Milioni 81.5 katika nafasi ya pili na nyota wa timu ya mpira wa kikapu ya Cleveland Cavaliers, LeBron James anayeingiza dola Milioni 77 katika nafasi ya tatu.
Orodha kamili ya wanamichezo 10 wanaoongozwa kulipwa kwa mujibu wa Forbes ni hii:
Wanamichezo 10 wanaolipwa zaidi kwa mujibu wa Forbes
NambaMuhusikaPato lake
1.Taylor SwiftDola Milioni 170
2.One DirectionDola Milioni 110 
3.James PattersonDola Milioni 95
=4.Cristiano RonaldoDola Milioni 88
=4.Dr. Phil McGrawDola Milioni 88
6.Kevin HartDola Milioni 87.5
7.Howard SternDola Milioni 85
8.Lionel MessiDola Milioni 81.5
9.AdeleDola Milioni 80.5
10.Rush LimbaughDola Milioni 79

Kwa mujibu wa Forbes, Ronaldo anapata Dola Milioni 55 kutokana na mshahara tu, wakati fedha nyingine zinatokana na mikataba yake ya udhamini. 
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United anafanya kazi na makampuni ya Nike, TAG Heuer, Sacoor Brothers Suits na Monster.
Si ajabu Mreno huyo kuongoza sasa kwa kipato hivi sasa, ikiwa hata uwanjani ameendelea kufanya vizuri na mwaka huu ukiingia katika moja ya miaka ya kukumb ukwa kwenye maisha yake ya soka.

Shaun Botterill/Getty Images
Huu ni mwaka wa kukumbukwa kwa Cristiano Ronaldo 
Mei mwaka huu alifunga penalti ya ushindi dhidi ya mahasimu wao wa Jiji, Atletico Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya wiki iliyopita kuiongoza Ureno kutwaa taji la Euro 2016 wakiwafunga wenyeji Ufaransa 1-0 katika fainali.




Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: