SIMBA, TFF WATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA DHAIRA


RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Uganda (FUFA) kaufuatia kifo cha mlinda mlango Abel Dhaira kilichotokea jana jijini Kampla.
Katika salamu hizo za rambirambi, Malinzi amewapa pole familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki, FUFA kufuatia msiba Dhaira, na kusema TFF ipo pamoja nao katika kipindi hiki cha maombelezo.
Dhaira alifariki jana Jumapili kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa Kansa
Wakati wa uhai wake Dhaira aliwahi kuidakia timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’ na kuvichezea vilabu vya Express FC, URA (Uganda), AS Vita (Congo DR), Simba SC (Tanzania) na klabu ya BV Vestmannaeyjar ya Iceland.
Abbel Dhaira (kushoto) siku za mwisho za uhai wake nchini Iceland

Wakati huo huo: Klabu ya Simba nayo imesema imepokea kwa mshtuko taarifa ya msiba wa mchezaji wake wa zamani mganda Abel Dhaira.
"Kwetu sisi ni pigo kubwa sana, ni msiba mzito sana, umetufanya tupate fadhaa kubwa, lakini hatuna la kufanya zaidi ya kumtakia mapumziko mema ya milele,".
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Hajji Manara amesema watamkumbuka sana Dhaira kwa uwezo wake wa kudaka krosi na nidhamu yake iliyokuwa mfano kwa wachezaji wote waliokuwepo kipindi kile.

"Tunawaomba familia ya marehemu iwe na subira kwenye kipindi hiki kigumu sana kwao,"amesema Manara.

Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: