LINDA NDOA YAKO MWANAMKE, ISIJE KUPONYOKA BURE!



Familia mseto kama hizi kupinduana hutokea sana


Unapoishi nyumbani na ndugu yako, jamaa yako au hata mtumishi wa kike, ni vizuri ukajitahidi kulinda ndoa yako. Kumbuka kwamba, wanaume hawajali hisia, hujali zaidi mwili. Kama ukimwachia ndugu yako, jamaa au rafiki yako kumzoea sana mumeo, jua tu kwamba, inawezekana unajitengenezea maumivu makubwa sana hapo baadae.

Tafiti zinathibitisha sana kwamba, mwanaume anapohisi kuwa mwanamke fulani anamwonesha kwamba, yeye ni mwanaume kweli kweli, anapoonesha kwamba, anatambua uwepo wake na mchango wake katika familia, mwanaume huanza kumpenda, bila kujali sura au hadhi.


Kama ndugu yako ni mjuaji wa mambo haya, anaweza kumwonesha mumeo kwamba, anaamini kuwa ni mwanaume kwelikweli. Hii hufanyika kwa kumsifu, kutopingana naye, kumpongeza mara kwa mara na kumwonesha kwamba anaamini katika yeye.


Hata wale watumishi wa ndani, wanaochukuliwa na wanaume za watu hawafanyi hivyo kwa sababu, ati hao watumishi ni wazuri sana wa sura au wanajua sana mapenzi, hapana.


Wanaume huwachukua kwa sababu, wake au wapenzi wa wanaume hao wameshindwa wajibu wao, wameshindwa kujua kwamba wanaume hutazama uhusiano kwa jicho tofauti.


Lakini, iwe ndugu au jamaa zenu na hata watumishi majumbani mwenu, bado na wao ni binadamu, wana udhaifu. Kwa udhaifu wao, pamoja na udhaifu wa wanaume au wapenzi wenu, wanaweza kuwasaliti. Kwa hiyo ni juu yenu kulinda ndoa zenu, ili udhaifu huo usiwe chanzo kwa kuvunjika kwa matumaini na matarajio yenu ya kujenga familia.


Kuna mambo mawili makubwa hapa, kwanza inawezwekana mmejiachia wazi sana kama wanawake na kusahau kuwa wanaume huvutiwa na mambo gani.


Kwa hali hiyo, mnawaacha wale walio karibu nao kuwafanyia yale wanayohitaji na kuchukua nafasi zenu.


Lakini pili, ni udhaifu wa kibinadamu na zaidi kwa wanaume, linapokuja suala la mwili. Kwa udhaifu huo, inabidi muwasaidie kuwalinda wasishawishiwe kirahisi. Lakini, ndugu zenu wa kike au watumishi mnaoishi nao, inabidi muwakague vizuri na kuacha kuwamini kupita kiasi kwa waume au wapenzi wenu.


Ni hatari sana kwa mwanamke kwa mfano, kumwambia au kumruhusu mumewe aende sehemu za starehe na rafiki yake wa kike au na ndugu yake wa kike, ati kwa sababu anamwamini rafiki huyo au mumewe. Kumbuka, suala hapa sio kuaminika au kutoaminika, bali ukweli wa kimaumbile pia. Mwanamke, chunga ndoa yako, ilinde sana, kwani sio dhambi.


Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: