lMPANGO WA FILIKUNJOMBE WILAYANI LUDEWA WAFANIKIWA.

Mpango wa mbunge wa jimbo laLudewa katika mkoa wa Njombekupitia chama cha mapinduzi Mh.Deo Filikunjombe wa kuwalipia ada za shule za Seokondari wanafunzi 25 kwa kila kata umefanikiwa kwa kiasi kikubwa hivyo kuwafanya wananchi wa jimbo hilo kuukubari na kumuomba kuendelea na utaratibu huo ambao umeweza kuwanufaisha wanafunzi walio wengi wanaotoka katika mazingira magumu.Mmoja wa wananchi wa kata ya Mavanga Bw.John Haule alisema kuwa awali kabla ya Filikunjombe kuingia madarakani watoto yatima walitegemea sana mashirika yasio ya kiserikali kuwasaidia katika kulipia gharama za masomo lakini haikusaidia lolote kwani mashirika yaliyo mengi hupata ufadhiri kwa miaka michache na miradi hiyo inapikwisha hali ilibaki kuwa mbaya kwa watoto hao tofauti na kipindi hiki.Bw.Haule alisema kuwa tokea alipoingia madarakani Filikunjombe ndani ya miaka mitano ameweza kuwalipia ada wanafunzi ambao wamefanikisha kuhitimu masomo yao kwa ngazi ya kidato cha nne na waliofanikiwa kufaulu ameendelea kuwapa msaada kwa kuwalipia ada katika ngazi ya kidato cha tano.Alisema wilaya ya Ludewa yenye kata 26 wameweza kusaidiwa zaidi ya wanafunzi 700 ambao mpaka sasa kuna wengine wameweza kujiunga nafani mbalimbali za ufundi baadaya kuhitimu kidato cha nne lakini kubwa zaidi wamekuwa wakikumbuka mchango wa mbunge wao katika maisha yao kwa kumpokea kwa shangwe nakumpa zawadi mbalimbali pale anapotembelea vijijini hali ambayo imemtia moyo mbunge huyo na kuona mpango wake umefanikiwa kwa kiasi kikubwa.“Mpango wa Filikunjombe umefanikiwa kwa asilimia miamoja kwani tumeanza kuyaona matunda yake lakini wakati anaanza na mpango huu wa kuwalipia ada wanafunzi wa mazingira magumu kwa kuwaagiza viongozi wa kata na vijiji kupendekeza majina ya watoto tuliona kama ni siasa leohii kila mmoja wetu ameona faida yake hivyo tunamuomba aendeleze mpango huu kwani niikombozi wakielimu katika wilaya yetu”,alisema Bw.Haule.Katibu wa Itikadi na uenezi wa chama cha Mapinduzi(CCM) mkoa wa Njombe Bw.Onoratus Mgaya katika ziara ya mbunge huyo kata za Mavanga,Ngelenge,Mawengi na Lupanga alisema kuwa chama cha mapinduzi kina hazina ya viongozi wachapa kazi akiwemoFilikunjombe hivyo wananchi wanapaswa kutambua umuhimu wa kuwaunga mkono vingozi wa namna hiyo.Bw.Mgaya alisema licha ya kuwalipia ada za shule watoto wa mazingira magumu pia Filikunjombe amekuwa ni mfanowa kuigwa nchini kwa kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi katika jimbo lake kwamuda muafaka hali ambayo imekuwa ikikipa sifa chama na kuwafanya wananchi kuendelea kukipa nafasi ya kuendelea kushika dora miaka mingi ijayo.Akihutubia katika mkutano wa hadhara kwa wananchi wa kata ya Mavanga Bw.Mgaya alisema kuwa CCM sio chama kibaya kamabaadhi ya wanasiasa wengine wanavyosema ila kunawatu wako ndani ya ccm ni wabaya na mkakati wa chama ni kuwaondoa watu hao haraka iwezekanavyo ili kusikiliza vilio vya wananchi kwani wananchi wanahitaji maendeleo na si porojo.Aidha akiongea na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mavanga Filikunjombe alisema kuwa mpango wake wa kuwalipia ada wanafunzi ulikuwa wa majaribio lakini kabla haja fanya utafiti wa majaribio yake ameshayaona mafanikio makubwa ambayo hakuyatarajia kutokana na kila kijiji anachopita amekuwa akipata mapokezi makubwa na zawadi kwa baadhi ya wanafunzi aliyowasaidia.Filikunjombe alisema licha ya kutoa msaada huo wa wanafunzi wenye mazingira magumu pia amekuwa akiwasisitiza wazazi kuwapeleka watoto shule ili mwisho wasiku waje kuwa viongozi wa wilaya hiyo kwani yeye si mbunge wa milele katikajimbo la Ludewa.Mwisho. @habari ludewa blog
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: