CHOMBEZO RAHA ZA BODA BODA sehem ya 2

Mage naye alijikokota hadi kituo cha daladala kutafuta usafiri wa Bajah “Anti twende dereva wa bodaboda alimwambia.. . “Nataka Bajaj, hakuna Bajaj hapa?” SONGA NAYO SASA . ……….. “Bajaj saa hizi wameshaondoka zao , twende na bodaboda ,” alisema kijana mmoja huku wenzake nao wakijaribu bahati zao kwa kumwita Mage akapande bodaboda zao . “Sitaki, ” alijibu kifupi huku akisimama kituoni kuangalia usafiri mwingine. Mara , Bajaj ilitoka upande wa Moroco , akaisimamisha na kupanda .. . “Kimara.” “Poa. ” Njiani, Mage alianza kumsimulia dereva wa Bajaj jinsi alivyomuoga kupanda bodaboda. .. “.. .tena nahisi hiyo siku nitakayopanda bodaboda nitaanguka mwenyewe bila kuangushwa ,” alisema Mage… “Anti hata mimi nakuunga mkono , unajua wale madereva wa bodaboda hawajitambui, wanachojua wao ni kwenda mbele tu lakini sheria za barabarani hawana habari nazo ,” alisema suka huyo . Mazungumzo yalichanganya mpaka wanafika Kimara ambako Mage alimwelekeza anapotakiwa kushuka … “Haya asante sana suka, ” alisema Mage baada ya kulipa, akaingia ndani kwake. Mage amekuwa mtu wa kuogopa bodaboda tangu shoga yake, Shungi alipopata nayo ajali akavunjika mguu na mkono mpaka sasa hayuko sawasawa. Hali hiyo ilimfanya Mage aape kwamba siku atakayopanda bodaboda lolote lile limpate na liwe fundisho kwake na kwa wengine . Mara zote inapotokea anataka kwenda mahali alitumia usafiri wa Bajaj , sanasana kama yuko sawa alitumia teksi lakini pia daladala ulikuwa usafiri wake mkubwa . Wiki moja ilipita, ikafika siku ya kikao kingine cha ile harusi , kulekule Kinondoni . Mage alijiandaa, siku hiyo alichelewa kidogo hivyo saa kumi na moja ndiyo alikuwa anatoka nyumbani . Pamoja na kuchelewa huko , Mage alilazimika kupanda Bajaj badala ya bodaboda kama alivyoshauriwa na mdogo wake, Joyce kwamba kwa sababu amechelewa angepanda bodaboda ili awahi.. . “Joy , mimi tangu lini nimepanda bodaboda, umesahau ya Shungi ?” “Wewe dada Mage bwana , kwani ajali si ajali tu ! Hujawahi kusikia mtu amepata ajali ya Bajaj ?” “Inatokea Joy lakini si kama ya bodaboda, bodi ni mwili wako .” Walicheka wote , Mage akaondoka zake ndani ya Bajaj kuelekea kwenye kikao. Kilikuwa ni kikao cha mwisho siku hiyo ambapo ilitakiwa kila mtu apangiwe majukumu kwa hiyo kilichukua muda mrefu sana .Mpaka saa sita juu ya alama usiku ikielekea siku nyingine , walikuwa bado wapo kikaoni. Saa saba kamili ndiyo walianza kutawanyika huku Mage akiwaza namna ya kutafuta Bajaj usiku huo , aliamini anaweza asipate… “Jamani mwenzenu leo sijui kama nitapata usafiri, ” Mage aliwaambia wajumbe wa kikao wakati wakitoka.. .“ Usafiri mbona wa kumwaga tu. Dar huwezi kukosa usafiri hata kidogo , ” alisema mjumbe mmoja , mama Saida. Mara , mvua ilianza kunyesha kwa mbali, Mage na wenzake wakakimbilia kwenye upenu wa nyumba kujificha .Mvua haikuwa kubwa wala ndogo, kati kwa kati kiasi kwamba, mama Saida alisema si mvua ya kukatika haraka … “Jamani kwa usiku huu , hii mvua haikatiki . Hii mpaka kunakucha. Afadhali twendeni, si tunakwenda majumbani mwetu ?”“Ni kweli ,” wengine waliunga mkono , wakaingia kwenye mvua. Kila mjumbe alipanda bodaboda , Mage alisita kwani alijua na mvua ile na akili za madereva wenyewe ndiyo kabisaaa ! Ajali nje nje ! Ilifika mahali kukawa kumetulia kabisa , Mage akajikuta anabaki peke yake baada ya bodaboda moja iliyokuwepo kituoni hapo kuanza kuondoka … “Anko .. .anko please ,” Mage alimwita dereva huyo .. . “Nipeleke Kimara mara moja . ” “Elfu kumi anti, si unaona mvua hii !” “Poa, lakini endesha polepole ,” alisema Mage huku akipanda. Hakuwa na namna kwani mvua nayo ilichanganya vibaya sana. “Suka .. .suka , unaona hapo mbele pana tuta, polepole bwana ,” alisema Mage huku macho yakiwa mbele kama yeye ndiye dereva .. . “Nimeona anti. Usiwe mwoga. ” “Nisiwe mwoga wakati maisha yangu nayaona yapo hatarini, we vipi?” “Anti kwani unadhani naweza kukuangusha?” “Kwa jinsi ninavyokuangalia hushindwi .” “Basi we ngoja nikuoneshe jinsi ya kukaa ili usiogope,” alisema suka akiweka pembeni bodaboda yake. Mage alikaa kuangalia pembeni , ile mikao ya wanawake wengi kwenye pikipiki au baiskeli. Suka akamwelekeza akae kama mwanaume amwangalie yeye. .. “Yeah ! Kaa hivyo, halafu nishike kiuno ili ujisapoti .” Mage alizungusha mikono yake na kuikutanisha mbele kwenye tumbo la dereva huyo .. . “Hapohapo , sasa utaona kama utaogopa . Unajua nyie wanawake mkipanda pikipiki huku mnaangalia pembeni ni rahisi sana kuangukia upande mwingine , lakini hapo sasa huwezi kuanguka, ” alisema suka huku akiongeza mwendo wa bodaboda . Mage aligundua ni kweli yuko salama kwa mkao huo kuliko ule wa mwanzoni . Kadiri spidi ya pikipiki ilipozidi , yeye alimlalia suka mgongoni na kukaza mikono kumkumbatia na hali hiyo pia ilimfanya akwepe manyunyu ya mvua na kuhisi kajoto f’lani hivi.. . Alijikuta akipeleka mikono hadi kuanza kushikashika flaizi .. . “Hee!” suka alipiga ukelele wa uendawazimu wa kidereva wa bodaboda …
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: