MBEYA WAZUA MAKUBWA BAAADA YA KUZIPIGA KUFULI OFISI ZA TENESCO

Wakazi wa jijini hapa jana walizua tafrani baada ya kufunga ofisi za Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco)kwa muda wakidai kupewa majibu kuhusu tatizo la upatikanaji wa umeme lililodumu kwa zaidi ya siku tano. Tukio hilo lilitokea jana saa 4:00 asubuhi baada ya wateja hao kusubiri majibu kutoka kwa wahusika, ambao awali walitangaziwa kuwa huduma hiyo ingeanza kupatikana juzi, lakini mpaka jana tatizo hilo lilikuwa likiendelea. Wakazi hao waliwafungia wafanyakazi wa Tanesco wa kitengo cha malipo, wakisema kuwa hawafanyi kazi yoyote na hivyo hawatakiwi kutoka nje. Hali hiyo ilidumu hadi askari wa walipowasili na kuwashauri waondoke. Wakizungumza kwa nyakati tofauti ofisini hapo, wateja hao walisema baada ya kukosekana kwa huduma ya luku kwa siku tatu, jana kupitia simu zao za mkononi walipokea ujumbe uliowataarifu kuwa huduma hiyo ingeanza kutolewa jana kwa mawakala na katika ofisi za Tanesco, hata hivyo hali haikuwa hivyo. Mkazi wa Mwanjelwa,Dickson Mwangungaalisema watendaji wa shirika hilo wanatoa taarifa zisizo sahihi na kusababisha usumbufu. “Ni vema kama wangetoa taarifa sahihi, watu tumefika hapa kwa ajili ya kununua umeme, lakini huduma hiyo haipo. Baadhi yao wanatuambia eti hali bado haijatengemaa, wengine wanasema tusubiri na muda unazidi kwenda, sasa nani mkweli? ndiyo maana tumeamua kuzifunga ofisi zao watupe jibu sahihi lini huduma hii itatengemaa,”:-Mwangunga. Hata hivyo, sakata hilo liliokolewa na mkuu wa upelelezi wa Wilaya ya Mbeya, Kitinkwi Mtatiro ambaye alifika katika ofisi hizo na kuwaomba wateja hao warejee nyumbani hadi watakapopewa taarifa ya kurejeshwa kwa huduma na uongozi wa Tanesco. “Nawaomba mfungue milango ya ofisi, waacheni wafanye kazi hili ni tatizo limetokea. Hata wao hawapendi karaha hii itokee ni vema mkawa watulivu msipende kujichukulia sheria mkononi. Jambo hili linaweza kuvuruga amani,”:-Mtatiro. Akizungumzia hali hiyo, meneja wa Tanesco wa Mbeya, Amos Maganga aliwaomba wananchi kuwa watulivu kwa kuwa tatizo hilo ni la kitaifa na mara mitambo itakaporekebishwa watajulishwa kupitia simu zao za mkononi. Jijini Dar es Salaam, wananchi waliendelea kulia na tatizo hilo lililodumu kwa siku tatu mfululizo. Baadhi yao wamelalamikia hasara wanayoipata kwa sababu ya kukosa umeme na kushindwa kufanya kazi za uzalishaji zinazotegemea uwapo wa umeme
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: