IMANI za kishirikina? Mshangao wa aina yake umetokea nyumbani kwa Miss Tanzania 2006 asiyechuja, Wema Abraham Sepetu ‘Madam’ baada ya kutupiwa hirizi getini kwake.
Wananchi wakishuhudia hirizi getini kwa Miss Tanzania 2006 asiyechuja, Wema Abraham Sepetu ‘Madam’.
Tukio hilo lililokusanya watu wapenda ‘ubuyu’ lilijiri alfajiri ya Jumamosi iliyopita, nyumbani kwa mlimbwende huyo, Kijitonyama-Bwawani jijini Dar baada ya mapaparazi wetu kutonywa juu ya uwepo wa tukio hilo.
TUJIUNGE NA CHANZO
“Njooni hapa kwa Wema tumekuta mfuko mweusi wa nailoni, ndani yake una hirizi, nazi zimeandikwa maandishi ya Kiarabu huku zikiwa zimevunjwavunjwa na pia kuna picha ya Diamond ndani yake,” kilisema chanzo hicho.
MAPAPARAZI WATIA TIMU
Mapaparazi wetu ambao walikuwa kwenye mizunguko yao kikazi, walitumia usafiri wa pikipiki kwenda nyumbani hapo ambapo ndani ya dakika ‘sifuri’ walikuwa wameshafika na kukuta vitu hivyo vikiwa vimezunguka na mashuhuda.
Wananchi wakizitazama kwa karibu zaidi hirizi hizo.
KILA MTU ASEMA LAKE
Wakati mapaparazi wetu walipokuwa wakidadisi juu nani aliyetupa kifurushi hicho na sababu za kufanya hivyo, mashuhuda hao kila mmoja alieleza lake.
“Sisi hatujui aliyetupa inaonekana atakuwa alikuja usiku sana lakini inaonesha mtupaji atakuwa anataka Wema na Diamond warudiane na ndiyo maana ameambatanisha na picha ya Diamond,” alisikika shuhuda mmoja huku mwingine akidakia:
“Aliyetupa hapa atakuwa ameweka zindiko ili Diamond asirudiane tena na Wema. Atakuwa anataka Diamond aendelee na Zari.”
Katika hali ya kushangaza, mlinzi wa kampuni moja inayolinda nyumbani kwa mlimbwende huyo, aliupiga teke na kuusambaratisha mfuko uliokuwa umehifadhi vitu hivyo pamoja na hirizi.
MAPAPARAZI WAMGONGEA WEMA
Ili kutaka kujua Wema amelichukuliaje tukio hilo, mapaparazi wetu waligonga geti la Wema ambapo alitoka binti mmoja ambaye hakutaka kujitambulisha jina lake na kuzungumza pasipo kufungua geti akiwa anachungulia kupitia uwazi mdogo uliopo getini hapo.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment