Nyota wa muziki wa bongo flava ambaye pia ni rais wa muziki huo, Diamond Platnumz anatarajia kuachia nyimbo nne kwa pamoja kabla ya mwezi March 2015ikiwepo collabo yake na mkali kutoka nchini DRC Congo, Fally Ipupa.
Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale amesema kuwa ziara ya Diamond barani Afrika imekuwa na mafanikio baada ya kukutana na wasanii wakubwa barani humu kama P-Square, Fally Ipupa,Flavour na wengine kitu kilichomfungulia milango hivyo kuweza kupata nafasi ya kufanya collabo na Fally Ipupa.
Aidha Babu Tale amesema kuwa kabla ya mwezi March mwaka huu watakuwa wameshaachia audio nne za Diamond ikiwepo collabo hiyo aliyofanya na Fally Ipupa.
Katika hatua nyingine Tale amesema kuwa baada ya kuachia nyimbo hizo video zitafuata na itajulikana zitafanyika wapi kama ni hapa kwa Adam Juma, GodFather au Moe Mussa.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment