Wakala wa wachezaji Mario Baloteli na Zlatan Ibrahimovic ameingia kwenye kinyang’anyiro cha kugombea urais wa FIFA huku upinzani mkubwa ukiwa kwa Rais wa sasa Sepp Blatter. Mino Raiola ambaye ana uraia wa Uholanzi atadhibitisha kuungwa mkono kwa vyama 5 vya soka na anategemewa kuakikisha kugombea kabla ya tarehe ya mwisho Januari 29.
Wakala huyo alipohojiwa na gazeti la ‘Daily Telegraph’ amesema anajisikia mgonjwa akiona Blatter anagombea tena Urais huo wa FIFA.
Wagombea wengine waliojitokeza kugombea kiti hicho ni Jerome Champagne na Makamo wa Rais wa chama cha soka barani Asia Prince Ali Bin Al-Hussein anetokea Jordan.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment