Bahanuzi aitahadharisha Yanga, Ataka kuifunga timu yake ya zamani

Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga, Said Bahanuzi, amewatahadharisha Yanga kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya timu yake ya sasa Polisi Morogoro mchezo unaosubiriwa kwa hamu kubwa kunako Uwanja wa Jamhuri. Bahanuzi ambaye ameenda Polisi Moro kwa mkopo katika dirisha dogo la Usajili, amesema kuwa kwa sasa anamapenzi na timu yake hiyo anayoitumikia kwa sasa hivyo amewataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kuangalia Yanga wakifia Jamhuri. “Wasitegemee kupata matokeo kirahisi, Tumejipanga kupata pointi tatu, Mashabiki wajekuona vijana nini tunacho” Amesema Bahanuzi. Yanga inayonolewa na kocha Hans Van Der Pluijm waliondoka jana Jijini Dar es salaam na kutua Morogoro tayari kwa mchezo huo hapo jioni ya leo ikiwa ni mchezo wa raundi ya 12 ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL).
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: