MTIBWA YALAZIMISHA SARE KWA STAND, JKT YAWACHAPA SHOOTING

Mtibwa Sugar imefanikiwa kupata sare katika Uwanja wake wa nyumbani wa Manungu Complex baada ya kusawazisha katika dakika za mwisho dhidi ya Stand United. Mtibwa ilisawazisha bao lake katika dakiak 10 za mwisho baada ya Stand kupata bao mapema kabisa. Mechi hiyo ilikuwa ni ya kiporo baada ya kuahirishwa jana kutokana na mvua kubwa kusababisha maji kujaa uwanjani. Kutokana na hali hiyo, mechi hiyo ilianza kuchezwa kuanzia dakika ya sita ambayo iliishia jana. WANAJESHI: Jana Ruvu Shooting walicheza dhidi ya ndugu zao Ruvu JKT katika mechi iliyopigwa usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar. JKT ndiyo walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao moja dhidi ya wapinzani na ndugu zao hao.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: