MAMBO MAPYA, MBEYA CITY KUUZA JEZI ZAKE KWA MTANDAO

Klabu ya Mbeya City imezindua rasmi njia mpya ya uuzaji wa jezi pamoja na sweta za klabu hiyo, kwa kuagiza kwa njia ya mtandao kisha kulipia benki yoyote hapa nchini inayotumia Visa kadi. Klabu hiyo msimu uliopita ilifanikiwa kuuza jezi kutokana na timu hiyo, kujizolea mashabiki wengi baada ya kuanza vyema ligi na kumaliza katika nafasi ya tatu lakini msimu huu inashika mkia kwenye ligi. Katibu wa timu hiyo, Emmnuel Kimbe, amesema wameamua kufanya hivyo ili kupunguza ule upenyo wa jezi feki kuzagaa mitaani. “ Tumezindua mpango wetu mpya wa uuzaji wa jezi na safari hii tumeleta na sweta ambazo shabiki popote pale alipo ndani au nje ya nchi ataweza kununua kwa njia ya mtandao akiwa na visa kadi ambayo ataitumia katika benki yoyote, jezi bei yake ni 20,000 na sweta 30,000. “Na hii tumefanya hivi kutokana na kupunguza lile wimbi la kuuza jezi ambazo sio halali,”alisema Kimbe.
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: