http://njenjenews.blogspot.com/#
Leo naomba tuwakumbuke bendi ya Magereza,Magereza Jazz
Bendi hii ipo mpaka sasa japo haina makali kama yale ya kipindi kile,hii ni mojawapo ya bendi za majeshi yetu ambazo zilitamba sana enzi zake sambamba na bendi nyingine za majeshi kama Air Jazz, Mwenge Jazz, Polisi Jazz, Uhamiaji Jazz, JKT Kimbunga Stereo, JKT Mafinga,Mzinga Troupe, Ruvu Jazz na nyinginezo.Bendi hii inamilikiwa na jeshi la Magereza Tanzania.Awali ilikuwa ikitumia mtindo wa Super Mnyanyuo(wana super mnyanyuo) na baadae(mwanzoni mwa miaka ya 90) walibadilisha mtindo na kuanza kutumia mtindo wa Mkote ngoma ambapo walianza kujulikana rasmi kama wana mkote ngoma,mtindo ambao wanautumia mpaka sasa.
Baadhi ya nyimbo za Magereza Jazz zilizotamba enzi hizo ni pamoja na Fatuma mwanangu, Ashura, Edina, Suzana, Nalala nakuota na nyingine nyingi(naomba tukumbushane hapa)
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kupitia bendi hii na kutamba nayo ni pamoja na hayati mzee John Kijiko, Abel Barthazar, Nanah Njige, Billy Mbwana, Ramadhan Mwerevu 'Choma choma', Issa Kamba, Issa Bendera, Wema Abdallah, Happy Siwea, Hamis Muyungwa, Stewart Singano 'Zozo', Gervas Herman, Hassan Kunyata na wengine wengi
Baadhi ya nyimbo za bendi hii zilizotamba sana ni pamoja na huu hapa chini wa Ashura
Ashura mimi najuta,
Mwenzenu kweli najuta sasa,
Visa ninavyofanyiwa na bwana huyu [Bwana huyu]
Nimeamini methali isemwayo [isemwayo]
Mkataa pema,
Oooh, pabaya panamwita x2
Leo hii mwenzenu ,
Kusema hivi mimi,
Nilimuacha mume wangu,nilidanganyika,
Kumuacha mume wangu, kumfuata bwana mwingine,
Kumbe ni mwizi baba, kumbe ni muongo.
Visa ninavyofanyiwa na bwana huyu [Bwana huyu]
Nimeamini methali isemwayo [isemwayo]
Mkataa pema,
Oooh, pabaya panamwita x2
Kibwagizo:
Nawausia wanawake wenzangu wote eeh,
Muheshimu ndoa zenu zisijevunjika x2
Muachane na mabwana wadanganyifu eeeh,
Atakupenda wakati una mumeo ooh,
Ukishaachika wala hana habari nawe
[Hana habari nawe]
Atakudanganya kwa curl na relaxer,
Atakudanyanya kwa khanga za Mombasa,
Atakudanganya kwa vitende vya Zaire,
Atakudanganya kwa chips na mayai,
Na starehe za muda hazina mwisho sikia
Nawausia wanawake wenzangu wote eeh,
Muheshimu ndoa zenu zisijevunjika x2
Wimbo mwingine wa Magereza Jazz uliotamba sana ni huu wa Edina.
karibu ndani karibu
mchumba wangu Edina njooo x 2
wala usiwe na wasiwasi
mimi bado sijaoa
usirudie mlangoni tu, hapa ni kwakoo
karibuuuuuuuu
(rudia mwanzo)
(wote) Kibwagizo
nakutegemea tuishi vyema kipenzi eh
nakutegemea tuishi vyema Edina
kwani silaha ya upendo ni tabia njema ahh mama X 2
sina bibi wala mke Edina ahh
wewe ni shada la ua ua
pokea penzi langu kwa mikono miwili
Edina chaguo langu mimi
(wote) kibwagizo
sina bibi wala mke Edina ahhh
wewe ni shada la ua la upendo
pokea penzi langu kwa mikono miwili
Edina chaguo langu mimi
(wote) kibwagizo
.................................................................................
Salama wakuu?.....
Leo naombeni tuwaangalie Bima Lee Orchestra....
Bendi hii ilianzishwa mwnzoni mwa miaka ya 80 na ilikuwa ikimilikiwa na Shirika la Bima la Taifa....Bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo kama Magnet 84 na baadaye Magnet ndele Tingisha(Magnet tingisha)..Bendi hii ilikuwa tishio kweli enzi hizo na ilipata nguvu zaidi mwaka 1984 baada ya kuwapata wanamuziki watano(05) Shaba Dede,Joseph Mulenga na Abdallah Gama(kutoka Mlimani Park orchestra) pamoja na Othman Momba na Jerry Nashon 'Dudumizi'(kutoka Vijana Jazz)....Wanamuziki hawa waliifanya Bima Lee Orchestra iibuke ghafla na kuwa tishio ikitumia mtindo wa Magnet 84....Hapa ndipo walitoka na nyimbo tamu kama Makulata,Neema,Tujemaso na nyinginezo...
Baadhi ya nyimbo zilizotamba sana na Bima Lee Orchestra ni pamoja na Makulata,Siri yako,Tujemaso,Frousie,Baba Shani,Samaki baharini,Visa vya Messenja,Ndoa Fungo la Hiyari,Dunia Ni Upepo,Busu Pande Tatu,Uzuri Ni Tabia, Penzi Dawa ya Chuki,Sitaki(visa vyako),Shakaza namba 2,Zenaba,Milionea wa mapenzi na nyinginezo nyingi.....
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kupitia bendi hii na kutamba nayo ni pamoja na Shaban Dede,Joseph Batholomeo Mulenga 'King Spoiler',Jerry Nashon 'Dudumizi',Abdallah Gama,Othman Momba,Rahma Shally,Stamili Uvuruge,Maxmillan(Max) Bushoke,Eddy Sheggy,Belesa Kakere,Suleiman Mwanyiro 'Computer',Roy Bashekanako,Jumbe Batamwanya,Shaban Lendi,Athuman Manicho,Stamili Uvuruge,Boniface Kachale,Lazaro Remmy,Muharami Said,Duncan Ndumbalo na wengine.
...............................................................................................
Kwa leo ngoja nimalize na DDC Mlimani Park Orchestra..........Dah....Hata sijui nianzie wapi hapa maana maelezo yatakuwa marefu kweli,ngoja japo niyafupishe kidogo....
Historia ya Bendi hii inaanzia mwaka 1978 ambapo takriban wanamuziki wanane waliihama bendi ya Dar International na
kwenda kuanzisha bendi ya Orchestra Mlimani Park.Baadhi yao ni aliyekuwa mtaalamu wa kupiga ala zote King MichaelEnock, Joseph Benard, Joseph Mulenga, Abdalah Gama, Cosmas Chidumule, Machaku Salum na Habib Jeff,hawa waliungana na Muhidin Maalim Gurumo,Hassan Rehani Bitchuka na Abel Barthazar(ambaye ndio hasa muanzilishi wa Mlimani Park)..... Ilijulikan hivyo(Mlimani Park Orchestra) kutokana kuwa na maskani yake pale Mlimani Club mitaa ya Mwenge jijini Dar es Salaam chini ya umiliki wa Tanzania Transport and Taxi Services.
Mwaka 1983 waliokuwa wamiliki wa bendi hiyo walifilisika na na hatimaye bendi hiyo ikachukuliwa na Dar es Salaam Development Corporation (DDC) na hapo ndiyo ikaanza kuvuma kwa jina la DDC Mlimani Park Orchestra ikiwa chini ya wanamuziki galacha na waasisi, Muhidin Maalim Gurumo, Abel Baltazar, Hassan Rehani Bitchuka, ambao walitokea JUWATA Jazz Band huku Cosmas Thobias Chidumule, Michael Enoch ‘King Michael’ na mpiga gitaa la solo mahiri, Joseph Batholemeo Mulenga, wakiwa wametwaliwa kutoka Dar International. ............Mtindo walioutumia tangu enzi hizo ni ule wa Sikinde Ngoma ya ukae.....
Baadhi ya nyimbo zilizotamba sana za Sikinde ni pamoja na Sauda/MV Mapenzi(namba 1 na 2),Neema,Usitumie Pesa kama fimbo,Mume wangu Jerry,Clara,Hiba,Matatizo ya nyumbani,Majirani huzima redio,Nidhamu ya kazi,Kassim amefilisika,Talaka ya hasira,Hadija,Barua toka kwa mama,Celina,Editha,Fikiri nisamehe,Pole mkuu mwenzangu,Diana,Pesa,Hata kama,Bubu ataka sema,Mnanionesha njia ya kwetu,Tangazia mataifa yote,Mtoto akililia wembe,Nalala kwa tabu,Duniani kuna mambo,Kiu ya jibu,Dua la kuku,Nawashukuru wazazi,Pata potea,Nelson Mandela,Uzuri wa mtu,mdomo huponza kichwa,Taxi Driver,Tucheze Sikinde,Conjesta na nyimbo niyngine nyingi tamu.....
Wanamuziki walioipitia bendi hii ni pamoja na King Michael Enock, Joseph Benard, Joseph Mulenga, Abdalah Gama, Cosmas Chidumule, Machaku Salum,Habib Jeff,Muhidin Maalim Gurumo,Hassan Rehani Bitchuka,Abel Barthazar,Henry Mkanyia,Fresh Jumbe,Hussein Jumbe,Benno Villa Anthony,Tino Masinge 'Arawa',Hassan Kunyata,Francis(Nassir) Lubua,Maalim Hassan Kinyasi,Abdallah Gama,Max Bushoke,Muharami Said,Kassim Mponda,Julius Mzeru,Said Chipelembe,Ally Jamwaka,Machaku Salum,Ally Yahaya,Shaban Lendi,Joseph Bernard,Juma Hassan Town na wengine wengi....
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
TWAKUM,BUKA
Wakati huo wa u "teen", mimi nilikuwa nikiwajua band iliyokuwa ikipiga pale Splendid, nna uhakika kuna watu wa Dar wazamani watapakumbuka hapo, The Rifters, walikuwa vijana wa Kariakoo, kinaDodger, Salah, Marehem Abdallah Matimbwa, na wengine siwakumbuki, tulikuwa tukienda siku za jumapili saa nane mchana (enzi hizo thubutu tutoke usiku) unaachiwa radhi!
Baada ya hao nawakumbuka "The Sunburst", enzi za bahari beach, ilikuwa raha sana siku za Jumapili tukienda family nzima anaetaka beach aende anaetaka mziki haya tena...
TWAKUMBUKA
Hawa Sunburst ndio hasa walianzisha huu mtindo unapjulikana sasa wa "mduara" kwenye dance za mziki wa kisasa. Nakumbuka walikuwa na nyimbo zao wakiziita za kitoto, kama vile "Ukuti" na mingineo ambayo kuikumbuka m kwa mara moja inakuwa shida.
Namkumbuka Muimbaji wao James, sijui yuko wapi huyu, nilimuona Kariakoo around 2005, halafu namkumbuka "Drummer boy" John Rocky, huyu yupo na namuona ona sana na baiskeli yake (hajabadilika in spite of age), na niliwahi muona miaka miwili mitatu nyuma akipiga drums pale Moevenpick halafu nikamuona Kempinski. Sijawahi kumuona Drummer boy better than him mpaka hii leo kwa huku kwetu. Namkumbuka pia mpiga wao bass maarufu Bashir, huyu ni mtoto wa yule mzee wa kizanzibari maarufu, gwiji la mziki Marehem Iddi farhan, inasemekana huyu Mzee Farhan watoto zake woote, zaidi ya kumi ni musicians (wakike na wakuime pamoja na mama yao) na inasemekana mpaka wafanyakazi wa nyumbani kwao (house girls na boys) nao pia ni musicians, isitoshe, mpaka majirani zao wengi wamefundishwa mziki na huyo mzee ama wanawe. Huyu Bashiri alikuwa na ndugu zake wanne Audu, Jaffar, Fresh na dada yao Jamila akipiga drums ) nilikuwa nikiwaona wakipiga ala tofauti hapo Sunburst.
Jamani hizo ni late 60s na 70s.
Nani anazikumbuka bendi hizi, za watoto wa mjini (in real sense)?
Hao jamaa wa The Sunburst nilichelewa kuwajua aisee.......Ila naambiwa walikuwa ni wazuri sana na ilikuwa ni bendi bora ya mwaka 1973......
Kingine ninachokijua kuhusu The Sunburst ni wimbo wao wa Banchikicha ambao mpaka sasa hurushwa kwenye vipindi vya zilipendwa vya vituo mbalimbli vy redio nchini.....
Pia najua kwamba kiongozi wa bendi hii alikuwa ni Kassim Magati
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Muigizaji huyu mkongwe mzee Majuto ametangaza kugombea ubunge jimbo la Tanga mjini.
Majuto mwenye umri zaidi ya miaka 60 ametangaza nia yake hiyo alipohojiwa na Clouds, na akadai atagombea kupitia CCM.
Bado tunamtafuta mzee majuto ili aweze kututhibitishia kama habari hizi ni kwa kweli au la na kama ni kweli ana mipango gani na jimbo hilo la Tanga mjini.
Je, kama ni kweli, unahisi ataweza ? Tupe maoni yako
Habari tulizozipata zinasema kuwa gwiji la sanaa za
vichekesho nchini, Amri Athumani 'King Majuto' ametangaza kugombea
ubunge kwa 2015.
< Scene ya mwisho aliyocheza marehemu Sharo Millionea na Kitale.
ROSE NDAUKA ATANGAZA RASMI KUZAA NJE YA NDOA
Staa wa filamu za Bongowood, Rose Ndauka ambaye ni mjamzito anadaiwa
kuwa atazaa kabla ndoa mwezi Aprili, mwakani. Akizungumza na mwanahabari
wetu, mchumbaa’ke, Malick Bandawe ambaye ni memba wa kundi la muziki la
TNG alianika aya za Kurani kuwa katika Dini ya Kiislamu si ruhusa
kufunga ndoa na mwanamke ambaye ni mjamzito kwani ni sawa na kufunga
ndoa na watu wawili hivyo anamsubiri ajifungue kwanza. “Ni kweli
mchumbaa’ngu hivi sasa ni mjamzito na anatarajia kujifungua mapema mwezi
wanne, mwakani. “Kuhusu kufunga naye ndoa kwa sasa ni ngumu hadi
ajifungue kwani kwa dini yetu (Uislam) si ruhusa kufanya hivyo lakini
atakapojifungua tu tutafunga ndoa,” alisema Malick. Malick ambaye hivi
sasa anatamba na Wimbo wa ‘Crazy Man’ alisema kuwa ana furaha kubwa
kuitwa baba mtarajiwa na anamuomba Mwenyezi Mungu Rose ajifungue salama
kwani anampenda kupita maelezo. Baada ya kuzungumza na Malick, gazeti
hili lilimtafuta mama wa Rose Ndauka, Batuli kufungukia ishu ya mwanaye
kubeba ujauzito kabla ya ndoa ambapo aligoma kuzungumza kwani
hakubaliani na suala hilo
Page under construction
Leo naomba tuwakumbuke bendi ya Magereza,Magereza Jazz
Bendi hii ipo mpaka sasa japo haina makali kama yale ya kipindi kile,hii ni mojawapo ya bendi za majeshi yetu ambazo zilitamba sana enzi zake sambamba na bendi nyingine za majeshi kama Air Jazz, Mwenge Jazz, Polisi Jazz, Uhamiaji Jazz, JKT Kimbunga Stereo, JKT Mafinga,Mzinga Troupe, Ruvu Jazz na nyinginezo.Bendi hii inamilikiwa na jeshi la Magereza Tanzania.Awali ilikuwa ikitumia mtindo wa Super Mnyanyuo(wana super mnyanyuo) na baadae(mwanzoni mwa miaka ya 90) walibadilisha mtindo na kuanza kutumia mtindo wa Mkote ngoma ambapo walianza kujulikana rasmi kama wana mkote ngoma,mtindo ambao wanautumia mpaka sasa.
Baadhi ya nyimbo za Magereza Jazz zilizotamba enzi hizo ni pamoja na Fatuma mwanangu, Ashura, Edina, Suzana, Nalala nakuota na nyingine nyingi(naomba tukumbushane hapa)
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kupitia bendi hii na kutamba nayo ni pamoja na hayati mzee John Kijiko, Abel Barthazar, Nanah Njige, Billy Mbwana, Ramadhan Mwerevu 'Choma choma', Issa Kamba, Issa Bendera, Wema Abdallah, Happy Siwea, Hamis Muyungwa, Stewart Singano 'Zozo', Gervas Herman, Hassan Kunyata na wengine wengi
Baadhi ya nyimbo za bendi hii zilizotamba sana ni pamoja na huu hapa chini wa Ashura
Ashura mimi najuta,
Mwenzenu kweli najuta sasa,
Visa ninavyofanyiwa na bwana huyu [Bwana huyu]
Nimeamini methali isemwayo [isemwayo]
Mkataa pema,
Oooh, pabaya panamwita x2
Leo hii mwenzenu ,
Kusema hivi mimi,
Nilimuacha mume wangu,nilidanganyika,
Kumuacha mume wangu, kumfuata bwana mwingine,
Kumbe ni mwizi baba, kumbe ni muongo.
Visa ninavyofanyiwa na bwana huyu [Bwana huyu]
Nimeamini methali isemwayo [isemwayo]
Mkataa pema,
Oooh, pabaya panamwita x2
Kibwagizo:
Nawausia wanawake wenzangu wote eeh,
Muheshimu ndoa zenu zisijevunjika x2
Muachane na mabwana wadanganyifu eeeh,
Atakupenda wakati una mumeo ooh,
Ukishaachika wala hana habari nawe
[Hana habari nawe]
Atakudanganya kwa curl na relaxer,
Atakudanyanya kwa khanga za Mombasa,
Atakudanganya kwa vitende vya Zaire,
Atakudanganya kwa chips na mayai,
Na starehe za muda hazina mwisho sikia
Nawausia wanawake wenzangu wote eeh,
Muheshimu ndoa zenu zisijevunjika x2
Wimbo mwingine wa Magereza Jazz uliotamba sana ni huu wa Edina.
karibu ndani karibu
mchumba wangu Edina njooo x 2
wala usiwe na wasiwasi
mimi bado sijaoa
usirudie mlangoni tu, hapa ni kwakoo
karibuuuuuuuu
(rudia mwanzo)
(wote) Kibwagizo
nakutegemea tuishi vyema kipenzi eh
nakutegemea tuishi vyema Edina
kwani silaha ya upendo ni tabia njema ahh mama X 2
sina bibi wala mke Edina ahh
wewe ni shada la ua ua
pokea penzi langu kwa mikono miwili
Edina chaguo langu mimi
(wote) kibwagizo
sina bibi wala mke Edina ahhh
wewe ni shada la ua la upendo
pokea penzi langu kwa mikono miwili
Edina chaguo langu mimi
(wote) kibwagizo
.................................................................................
Salama wakuu?.....
Leo naombeni tuwaangalie Bima Lee Orchestra....
Bendi hii ilianzishwa mwnzoni mwa miaka ya 80 na ilikuwa ikimilikiwa na Shirika la Bima la Taifa....Bendi hii ilikuwa ikitumia mitindo kama Magnet 84 na baadaye Magnet ndele Tingisha(Magnet tingisha)..Bendi hii ilikuwa tishio kweli enzi hizo na ilipata nguvu zaidi mwaka 1984 baada ya kuwapata wanamuziki watano(05) Shaba Dede,Joseph Mulenga na Abdallah Gama(kutoka Mlimani Park orchestra) pamoja na Othman Momba na Jerry Nashon 'Dudumizi'(kutoka Vijana Jazz)....Wanamuziki hawa waliifanya Bima Lee Orchestra iibuke ghafla na kuwa tishio ikitumia mtindo wa Magnet 84....Hapa ndipo walitoka na nyimbo tamu kama Makulata,Neema,Tujemaso na nyinginezo...
Baadhi ya nyimbo zilizotamba sana na Bima Lee Orchestra ni pamoja na Makulata,Siri yako,Tujemaso,Frousie,Baba Shani,Samaki baharini,Visa vya Messenja,Ndoa Fungo la Hiyari,Dunia Ni Upepo,Busu Pande Tatu,Uzuri Ni Tabia, Penzi Dawa ya Chuki,Sitaki(visa vyako),Shakaza namba 2,Zenaba,Milionea wa mapenzi na nyinginezo nyingi.....
Baadhi ya wanamuziki waliowahi kupitia bendi hii na kutamba nayo ni pamoja na Shaban Dede,Joseph Batholomeo Mulenga 'King Spoiler',Jerry Nashon 'Dudumizi',Abdallah Gama,Othman Momba,Rahma Shally,Stamili Uvuruge,Maxmillan(Max) Bushoke,Eddy Sheggy,Belesa Kakere,Suleiman Mwanyiro 'Computer',Roy Bashekanako,Jumbe Batamwanya,Shaban Lendi,Athuman Manicho,Stamili Uvuruge,Boniface Kachale,Lazaro Remmy,Muharami Said,Duncan Ndumbalo na wengine.
...............................................................................................
Kwa leo ngoja nimalize na DDC Mlimani Park Orchestra..........Dah....Hata sijui nianzie wapi hapa maana maelezo yatakuwa marefu kweli,ngoja japo niyafupishe kidogo....
Historia ya Bendi hii inaanzia mwaka 1978 ambapo takriban wanamuziki wanane waliihama bendi ya Dar International na
kwenda kuanzisha bendi ya Orchestra Mlimani Park.Baadhi yao ni aliyekuwa mtaalamu wa kupiga ala zote King MichaelEnock, Joseph Benard, Joseph Mulenga, Abdalah Gama, Cosmas Chidumule, Machaku Salum na Habib Jeff,hawa waliungana na Muhidin Maalim Gurumo,Hassan Rehani Bitchuka na Abel Barthazar(ambaye ndio hasa muanzilishi wa Mlimani Park)..... Ilijulikan hivyo(Mlimani Park Orchestra) kutokana kuwa na maskani yake pale Mlimani Club mitaa ya Mwenge jijini Dar es Salaam chini ya umiliki wa Tanzania Transport and Taxi Services.
Mwaka 1983 waliokuwa wamiliki wa bendi hiyo walifilisika na na hatimaye bendi hiyo ikachukuliwa na Dar es Salaam Development Corporation (DDC) na hapo ndiyo ikaanza kuvuma kwa jina la DDC Mlimani Park Orchestra ikiwa chini ya wanamuziki galacha na waasisi, Muhidin Maalim Gurumo, Abel Baltazar, Hassan Rehani Bitchuka, ambao walitokea JUWATA Jazz Band huku Cosmas Thobias Chidumule, Michael Enoch ‘King Michael’ na mpiga gitaa la solo mahiri, Joseph Batholemeo Mulenga, wakiwa wametwaliwa kutoka Dar International. ............Mtindo walioutumia tangu enzi hizo ni ule wa Sikinde Ngoma ya ukae.....
Baadhi ya nyimbo zilizotamba sana za Sikinde ni pamoja na Sauda/MV Mapenzi(namba 1 na 2),Neema,Usitumie Pesa kama fimbo,Mume wangu Jerry,Clara,Hiba,Matatizo ya nyumbani,Majirani huzima redio,Nidhamu ya kazi,Kassim amefilisika,Talaka ya hasira,Hadija,Barua toka kwa mama,Celina,Editha,Fikiri nisamehe,Pole mkuu mwenzangu,Diana,Pesa,Hata kama,Bubu ataka sema,Mnanionesha njia ya kwetu,Tangazia mataifa yote,Mtoto akililia wembe,Nalala kwa tabu,Duniani kuna mambo,Kiu ya jibu,Dua la kuku,Nawashukuru wazazi,Pata potea,Nelson Mandela,Uzuri wa mtu,mdomo huponza kichwa,Taxi Driver,Tucheze Sikinde,Conjesta na nyimbo niyngine nyingi tamu.....
Wanamuziki walioipitia bendi hii ni pamoja na King Michael Enock, Joseph Benard, Joseph Mulenga, Abdalah Gama, Cosmas Chidumule, Machaku Salum,Habib Jeff,Muhidin Maalim Gurumo,Hassan Rehani Bitchuka,Abel Barthazar,Henry Mkanyia,Fresh Jumbe,Hussein Jumbe,Benno Villa Anthony,Tino Masinge 'Arawa',Hassan Kunyata,Francis(Nassir) Lubua,Maalim Hassan Kinyasi,Abdallah Gama,Max Bushoke,Muharami Said,Kassim Mponda,Julius Mzeru,Said Chipelembe,Ally Jamwaka,Machaku Salum,Ally Yahaya,Shaban Lendi,Joseph Bernard,Juma Hassan Town na wengine wengi....
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
TWAKUM,BUKA
Wakati huo wa u "teen", mimi nilikuwa nikiwajua band iliyokuwa ikipiga pale Splendid, nna uhakika kuna watu wa Dar wazamani watapakumbuka hapo, The Rifters, walikuwa vijana wa Kariakoo, kinaDodger, Salah, Marehem Abdallah Matimbwa, na wengine siwakumbuki, tulikuwa tukienda siku za jumapili saa nane mchana (enzi hizo thubutu tutoke usiku) unaachiwa radhi!
Baada ya hao nawakumbuka "The Sunburst", enzi za bahari beach, ilikuwa raha sana siku za Jumapili tukienda family nzima anaetaka beach aende anaetaka mziki haya tena...
TWAKUMBUKA
Hawa Sunburst ndio hasa walianzisha huu mtindo unapjulikana sasa wa "mduara" kwenye dance za mziki wa kisasa. Nakumbuka walikuwa na nyimbo zao wakiziita za kitoto, kama vile "Ukuti" na mingineo ambayo kuikumbuka m kwa mara moja inakuwa shida.
Namkumbuka Muimbaji wao James, sijui yuko wapi huyu, nilimuona Kariakoo around 2005, halafu namkumbuka "Drummer boy" John Rocky, huyu yupo na namuona ona sana na baiskeli yake (hajabadilika in spite of age), na niliwahi muona miaka miwili mitatu nyuma akipiga drums pale Moevenpick halafu nikamuona Kempinski. Sijawahi kumuona Drummer boy better than him mpaka hii leo kwa huku kwetu. Namkumbuka pia mpiga wao bass maarufu Bashir, huyu ni mtoto wa yule mzee wa kizanzibari maarufu, gwiji la mziki Marehem Iddi farhan, inasemekana huyu Mzee Farhan watoto zake woote, zaidi ya kumi ni musicians (wakike na wakuime pamoja na mama yao) na inasemekana mpaka wafanyakazi wa nyumbani kwao (house girls na boys) nao pia ni musicians, isitoshe, mpaka majirani zao wengi wamefundishwa mziki na huyo mzee ama wanawe. Huyu Bashiri alikuwa na ndugu zake wanne Audu, Jaffar, Fresh na dada yao Jamila akipiga drums ) nilikuwa nikiwaona wakipiga ala tofauti hapo Sunburst.
Jamani hizo ni late 60s na 70s.
Nani anazikumbuka bendi hizi, za watoto wa mjini (in real sense)?
Hao jamaa wa The Sunburst nilichelewa kuwajua aisee.......Ila naambiwa walikuwa ni wazuri sana na ilikuwa ni bendi bora ya mwaka 1973......
Kingine ninachokijua kuhusu The Sunburst ni wimbo wao wa Banchikicha ambao mpaka sasa hurushwa kwenye vipindi vya zilipendwa vya vituo mbalimbli vy redio nchini.....
Pia najua kwamba kiongozi wa bendi hii alikuwa ni Kassim Magati
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Mzee Majuto atangaza kugombea ubunge mwaka 2015
Muigizaji huyu mkongwe mzee Majuto ametangaza kugombea ubunge jimbo la Tanga mjini.
Majuto mwenye umri zaidi ya miaka 60 ametangaza nia yake hiyo alipohojiwa na Clouds, na akadai atagombea kupitia CCM.
Bado tunamtafuta mzee majuto ili aweze kututhibitishia kama habari hizi ni kwa kweli au la na kama ni kweli ana mipango gani na jimbo hilo la Tanga mjini.
Je, kama ni kweli, unahisi ataweza ? Tupe maoni yako
07.10.2013 - Tags:
Majuto
< Scene ya mwisho aliyocheza marehemu Sharo Millionea na Kitale.
div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
ROSE NDAUKA ATANGAZA RASMI KUZAA NJE YA NDOA
Page under construction