MWANZO MWEMA WA KINGSTONE FC KWENYE MASHINDANO YA KUAMBIANA CUP - LUDEWA
Kwa mara ya kwanza katika historia ya timu ya Kingstone FC yenye makazi yake katika kijiji cha Lihagule, wanashiriki mashindano ya Kuambiana Cup yanayofanyika Ludewa. Hii ni hatua kubwa kwa timu hiyo changa ambayo imeibuka kufuatia mpasuko ndani ya timu ya zamani ya Lihagule FC.
Leo Kingstone FC wanakabiliwa na kibarua kigumu dhidi ya Idusi FC, timu ambayo haijawahi kuwa na mafanikio makubwa katika mashindano haya, lakini safari hii inatarajiwa kuja na mwamko mpya. Hii inatokana na ujio wa wakazi wapya kutoka maeneo ya shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe, ambao huenda wakawa chachu ya mabadiliko ndani ya timu ya Idusi.
Kijiji cha Lihagule kinatambulika zaidi kwa mchezo wa ngoma ya asili ya Mganda, lakini sasa kimegeuka kuwa kitovu cha ushindani wa soka kufuatia kuanzishwa kwa Kingstone FC. Je, timu hii mpya itaandika historia kwa mafanikio yao ya mwanzo?
Mashabiki wanatarajia kuona mechi kali kwenye Uwanja wa Masasi, ambapo pambano hili linaelezwa kuwa la kipekee na la kuvutia.
Kwa mujibu wa takwimu za awali, Kingstone FC wameshushwa na wataalamu kwa Odds ya 1.10 huku Idusi FC wakipewa Odds ya 1.50 – hali inayoonyesha matarajio makubwa kwa Kingstone kuibuka na ushindi.
Mashabiki wa soka Ludewa wasubiri burudani ya aina yake!
0 comments:
Post a Comment