SASHA: NAOLEWA KUTOA NUKSI







 
Sasha Kassim.
MWANADADA mwenye mvuto wa aina yake Bongo, Sasha Kassim ambaye anatarajia kufunga ndoa mwanzoni mwa mwaka kesho amesema kuwa, ameamua kuolewa ili kutoa nuksi.

Sasha ambaye hujulikana sana mitandaoni kwa picha zake za kihasara, alisema hadi sasa bado hajaenda kutambulishwa ukweni na wala hakuna mpango huo, ila amekuwa akiwasiliana na wakwe zake kwa njia ya simu, baada ya ndoa ndipo ataenda kupata baraka zao lakini makazi yake yataendelea kuwa Bongo.

“Naolewa kutoa nuksi si unajua mwanamke kukaa bila ndoa haileti picha nzuri, wakwe zangu wamenikubali japo hawajawahi kuniona laivu zaidi ya kwenye simu, nimeshaongea na mume wangu mtarajiwa kwamba akinioa nitaendelea kuishi Bongo, sababu napapenda sana huko Italy nitakuwa naenda kwa muda mfupi na kurudi na amekubali,” alisema Sasha ambaye anatarajia kuolewa na Bonphace, raia wa Italy.


Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: