WAALGERIA WAPEWA RUNGU KUZIAMUA TAIFA STARS,NIGERIA AFCON

Cairo,Misri.
SHIRIKISHO la Soka Afrika,CAF,leo limemtangaza Mwamuzi,Mehdi Abid Charef,kutoka nchini Algeria kuwa ndiye atakayechezesha mchezo wa marudiano wa kundi G wa kuwania tiketi ya kufuzu michuano ya AFCON kati ya wenyeji  Nigeria dhidi ya wageni Tanzania (Taifa Stars).
Mbali ya Charef waamuzi wengine waliopewa jukumu la kuchezesha mchezo huo ambao nao ni kutoka nchini Algeria ni Abdelhak Etchiali na Ahmed Tamen.Mustapha Ghorbal atakuwa mwamuzi wa akiba.Kamisaa/Kamishna wa mchezo huo atakuwa Inyangi Bokinda kutoka nchini Congo DRC.
Tanzania na Nigeria zinatarajiwa kurudiana Septemba 3,2016 katika uwanja wa Adokiye Amiesiamaka ulioko katika mji wa Port Harcourt.Mchezo huo utakuwa ni wa kukamilisha ratiba kwani tayari timu zote mbili zimeshindwa kufuzu baada ya kumaliza nyuma ya vinara Misri.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Dar Es Salaam miezi kadhaa iliyopita timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bila kufungana.



Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: