DONE DEAL:JOEL CAMPBELL AIHAMA ARSENAL


Lisbon,Ureno.
SHAMBULIAJI wa kimataifa wa Costa Rica,Joel Campbell,ameihama Arsenal na kujiunga na Sporting Lisbon ya Ureno kwa mkataba wa mkopo wa msimu mmoja.
Campbell,24,amejiunga na Sporting Lisbon baada ya kushindwa kuhakikishiwa namba katika kikosi cha kwanza cha Arsenal licha ya kufanya vizuri katika michezo ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu.
Hii ni mara ya tano sasa kwa Campbell kuihama Arsenal kwa mkopo tangu alipojiunga nayo mwaka 2011 akitokea Derportiva Saprisa ya nyumbani kwao Costa Rica.
Campbell anaiacha Arsenal kwa mara nyingine akiwa ameichezea jumla ya michezo 40 na kuifungia mabao manne katika michuano yote.




Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: