MANENO MATATU MAZITO YA MOURINHO JUU YA ZLATAN IBRAHIMOVIC


Kocha wa Manchester Jose Mourinho amemuelezea kwa maneno matatu straika wake mpya Zlatan Ibrahimovic.
Mreno huyo amefanikiwa kumnasa mchezaji huyo wa zamani wa Inter Milan, Barcelona, AC Milan Paris Saint-Germain kwenye dirisha hili la usajili baada ya kumaliza kazi iliyompeleka nchini Ufaransa akiwa na PSG.
Wawili hao walipata wakati murua sana walipokuwa Inter Milan, na Mourinho amekanusha vikali kwamba straika huyo ni mtu mwenye maringo na majivuno makubwa.
“Nina maneno matatu tu ya kumwelezea Zlatan, ni mshindi, mfungaji hodari na vile vile ni mcheshi,” amesema Mourinho..
“Unahitaji kumwelewa kwa uzuri. Ni mcheshi sana na kama humfahamu vizuri, halafu ukasikiliza na kusoma nukuu zake basi unaweza kudhani ni mtu mwenye majivuno makubwa sana. 
“Lakini ukweli ni kwamba, Zlatan ni mtu mcheshi sana. Hivyo naweza kusema kwamba, ni mcheshi, mshindi na mfungaji. Nimekuwa na furaha sana kumpata, na ni dhahiri kwamba yeye pia ana furaha kubwa kufanya kazi na mimi.”
- See more at: http://www.njenjenews.blogsport.com/2016/07/maneno-matatu-mazito-ya-mourinho-juu-ya.html#sthash.xRftPstu.g7hCsvao.dpuf



Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: