AZAM FC NAYO YALETA MZIMBABWE, NI MKALI WA MABAO BRUCE KANGWA


NYOTA wa Kimataifa ya Zimbabwe, Bruce Kangwa, ametua nchini jioni ya leo tayari kabisa kufanya majaribio ya kujiunga na Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC.
Kangwa anatokea kwa vinara wa Ligi Kuu nchini humo Highlanders FC na mpaka sasa ligi hiyo ikiwa mapumzikoni kufuatia kumaliza mzunguko wa kwanza, amefanikiwa kuwa kileleni kwa ufungaji bora akiwa na mabao saba.
Mzimbabwe huyo ameshachezea timu yake ya Taifa mechi 20 na mpaka sasa yupo kwenye kikosi hicho na anamudu kucheza nafasi tatu tofauti uwanjani, beki wa kushoto, winga wa kushoto na mshambuliaji.
Akizungumza mara baada ya kuwasili nchini jana, Kangwa alisema kuwa amejipanga kufanya vizuri kwenye majaribio hayo.

Bruce Kangwa akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam jana

“Ninajisikia vizuri sana nikiwa mchezaji wa kigeni kupata nafasi ya kujaribiwa na Azam FC, haya ni  mafanikio makubwa sana, mchezaji wa Zimbabwe kuja hapa kwa majaribio ni mafanikio kwani kuna wachezaji wengi hata katika nchi nyingine, niko hapa kuonyesha uwezo wangu nina uhakika nitafanikiwa kusajiliwa,” alisema.
Kangwa, 27, anaungana na wachezaji waliokuwa kwenye majaribio, beki Mohamed Chicoto (Niger), washambuliaji Ibrahima Fofana (Ivory Coast), Fuadi Ndayisenga (Burundi) na Mossi Moussa Issa (Niger).

Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: