LIVERPOOL YAWANIA KUMSAINI GOTZE!



KLOPP-GOTZELiverpool wana nia ya kumsaini Mchezaji wa Bayern Munich Mario Gotze kwa mujibu wa vyanzo toka huko England.
Gotze, Kiungo wa Miaka 23, anahusishwa na kujiunga na Liverpool hasa kwa vile Meneja wa sasa wa Klabu hiyo, Jurgen Klopp, alikuwa pamoja na Mchezaji huyo walipokuwa wote Klabu ya Borussia Dortmund huko Germany.
Gotze, ambae ndie alifunga Bao pekee na la ushindi kwenye Fainali ya Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014 Germany ilipoifunga Argentina 1-0, amekuwa hana namba huko Bayern chini ya Kocha Pep Guardiola na hajaanza Mechi tangu Oktoba.
Guardiola sasa atajiunga na Manchester City mwishoni mwa Msimu na Bayern kuwa chini ya Carlo Ancelotti huku hatima ya Gotze ikiwa njia panda na akiwa amebakisha Mwaka mmoja tu kwenye Mkataba wake na Bayern.
Mchezaji huyo aling’ara mno alipokuwa na Klopp huko Dortmund tangu Meneja huyo ampe namba kwa mara ya kwanza Mwaka 2010 alipokuwa na Miaka 18 tu.
Chini ya Klopp, Gotze aliichezea Dortmund Mechi 99 na kufunga Bao 22 kabla kuhamia Bayern Mwaka 2013 kwa Dau la Pauni Milioni 31.5.
Inaaminika Liverpool wanaamini wanaweza kumsaini Gotze kwa Dau la Pauni Milioni 20 hasa ukizingatia muda wa Mkataba wake na Bayern uliobakia.
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba
**Saa za Bongo
Jumamosi Aprili 2
1445 Aston Villa v Chelsea
1700 Arsenal v Watford              
1700 Bournemouth v Man City    
1700 Norwich v Newcastle          
1700 Stoke v Swansea               
1700 Sunderland v West Brom    
1700 West Ham v Crystal Palace  
1930 Liverpool v Tottenham                 
Jumapili Aprili 3
1530 Leicester v Southampton    
1800 Man United v Everton

Ludewa yetu na maendeleo yetu
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: