i wish you happy chrismass and happy new year
Hapa kijana BENNY amepiga magoti kutokana na ulemavu unaomkabili |
Kijana benny ni mlemavu wa miguu tangu miaka mingi iliyopita kijana huyo anaishi katika kijiji cha amani kata ya mundindi katika wilaya ya ludewa mkoa wa njombe haliyake ni ngumu saana hasa katika suala la malazi na usafiri juu ya tatizo lake kwakuwa mpaka sasa mlemavu huyo hana wazazi kutokana na wazazi wake wote wawili kutangulia mbele ya haki.
Mlemavu huyo anatembea kwa kutambaa ili kufika kila semu anakohitaji kufika kutokana na halingumu aliyokuwanayo hivyo inamlazimu kufanya hivyo licha ya kuwa anateseka saana hasa kwa kutumia mikono yake miwili kama miguu.
Hata hivyo kijana huyo hanauwezo wa kuzungumza maneno ya kueleweka anazungumza kwa shida saana wakati mwingine hulazimika kukaa karibu na mtu au kitu anacho kihitaji iliawezekupata msaada.
Mmiliki wa mtandao huu Bw, Maiko luoga aliweza kufika katika kijiji hicho na kukutana na kijana huyo hivyo kujionea halihalisi juu ya maisha ya mateso anayopata mlemavu huyo na kufanya uamuzi wa kuzisambaza habari hizi katika mitandao ya kijamii ili kijana huyo aweze kusaidiwa.
Kwasasa kijana huyo anatunzwa na wajomba zake ndio ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa kijana huyo hivyo wajomba zake walisema kuwa kama kijana wao angepata msaada wa aina yoyote ingekuwa msaada mkubwa saana kwa kijana benny.
Hata hivyo kwa yeyote aliyeguswa na kijana huyo anaweza kuwasiliana na mtandao huu kupitia namba za simu 07 6270 5839/ 06 5560 5839 ili kuweza kumsaidia kijana huyu.
0 comments:
Post a Comment