CHOMBEZO; HEHEEE, KANTANGAZEEE!!! SEHEMU YA KUMI NA MBILI


0718603654

Ninaamka asubuhi ninajiona kitandani nipo peke yangu nimezongwa na shuka tu! Ninainuka ninakaa kitako kwa muda, lakini Baby simuoni kurejea kitandani. Ninasubiri labda amekwenda chooni, lakini muda mrefu unakatika Baby harudi. Ninakwenda chooni kumtazama napo patupu. Bafuni patula! Akili inanirufaa!!!
“Baby, halow, Baby uwapi?!.”
Ninamwita huku nikiwa nimepagawa!

***
Meneja baada yakutoka kwa Dobe, amekwenda kazini kwake, akafungua ofisi yake, kisha akawatolea mafuta wafanyakazi wake akawakabidhi. Akakaa kwenye kiti hana raha hata kidogo. Mawazo yamemtinga sana. Anawaza namna ipi afanye ili amuamishe Dobe, kutoka kwa Baby Mwanamtama. Awe katika himaya yake. Mara yakapita mawazo kuwa amtafute dalali ili amtafutie nyumba atakayomuweka Dobe, kisha atakuwa anavinjari raha zake kwa utuo. Kwani kwa umbile lake, inakuwa tabu sana kutongozwa na wanaume. Hata wale waliokuwa na roho ngumu, huamua kumuonesha dalili tu kuwa wanamtaka lakini hawathubutu kumtamkia bayana.
Meneja anatoa simu yake anaibonyeza anaitafuta namba ya dalali, na hatimae anaiona anampigia.
Dalali anapopokea simu yake, anazungumza nae kwa kina.
“Sasa, ninataka nyumba ambayo iwe ni upande au chumba na varanda unavyo? Lakini choo chake kijitegemee”
Dalali anaitikia kuwa anavyo. Meneja anamwita aende ofisini kwake akimueleza kuwa kuna mtu anataka kwenda kuviona.
Dalali anamwambia hakuna shida anakwenda. Dalali huyu wanafahamiana sana kwani hata nyumba waliyowekea ofisi, yeye ndiyo aliyowatafutia.
Meneja anakata simu, kisha anatabasamu. Anabonyeza namba za Dobe, ili amfahamishe lakini Dobe simu yake haipatikani. Anajaribu tena na tena, lakini hali haibadiliki inakuwa ni vilevile. Anaamua kutuma ujumbe, ili simu ile ikiwashwa tu, kwake utaingia ujumbe wa kupokelewa ujumbne wake.
Dadali amewasili lakini dobe hapatikani kwenye simu.
Meneja akamueleza kuwa mtu anaetaka kwenda kutazama vyumba, ametoka hivyo afanye subira kidogo. Dalali amekaa kila muda anatazama saa yake.
“Sasa mie wenzangu wanafanya kazi, mie ninazururishwa tu kuja hadi huku kisha muhitaji wa chumba hayupo, hii si dharau hii?!”
Dalali analalamika kwa meneja. Meneja anamsihi atulie pesa za kumuweka atamlipa ila leo kabla ya kesho wapate hivyo vyumba. Wakiwa katika kuzungumza na Dalali, Meneja anaijaribu tena simu ya Dobe lakini bado imezimwa.
Meneja kuna mtu anamuona anaingia katika ofisi yao ili kuweza kupata huduma, meneja anaamua kuachana na ile simu, anampokea mteja.
“Dada habari yako?”
Meneja anasalimiwa na mteja.
“Njema karibu Njasi.”
“Ninataka huduma lakini ninaomba nihudumiwe na Dobe, anajua sana kuhudumia.”
Njasi anamwambia meneja kwa sauti inayoonesha anajambo la ziada.
Meneja anachukia sana wivu unamtawala, unamsugua ndani ya roho yake.
“Samahani mteja wetu, Dobe leo anaumwa hajaja kazini, amelala nyumbani kwake ila siku zijazo atakuwapo, atakapokuwa amepata unafuu. Ingawa pia hatakaa kwenye nafasi yake ya awali, kwani sasa Dobe ni naibu Meneja. Hivyo ninakuomba uwakubali na wahudumu wetu wengine wakuhudumie nao pia ni mahiri sana.”
Maneno hayo ya meneja yanamtia sana ganzi Njasi.
“Ooooo masikini, hebu nielekeze nikimaliza kufanyiwa Massage nikamkague, kwani kuna kitu aliniagiza.”
Njasi anaongopa ili aelekezwe kwa Dobe kwani hata ujaji wake hapa alikuwa ni maalum kwa kutimiziwa haja yake, leo alikuwa hataki kuremba!
Meneja ndani ya moyo wake anachukia sana hana namna tu. Meneja anamuelekeza Njasi anapoishi Dobe, akiamini kesho tu, Dobe atamuingiza katika nyumba nyingine, akiwa chini ya himaya yake.
“Ok sawa nimeelewa vizuri tu, sasa acha kwanza nikamuone huko alipo, nitakuja kufanya massage baadae.”
Njasi anaondoka ofisini kwa Meneja, anampigia simu shoga yake Qeenlyn.
Simu inapopokelewa upande wa pili Njasi anamuuliza shoga yake kama ana nafasi wakutane Tabata Bima ana bonge la story amwambie.
Qeenlyn akamwambia nae yupo maeneo ya Tabata kwa mfojo, anapata supu. Wakakubaliana wakutane mahala hapo.
Njasi akasafiri hadi Tabata Chama kwa Mfojo, akitumia usafiri wa bajaji, akakutana na shoga yake.
“Shoga nikupe ubuyu, nimempata bwana huyo ni hatari sijapata kuona na utundu wangu wote! Yaani amenimaliza hadi kwenye maini.”
Njasi anampa ubuyu shoga yake, aliekuwa akimsikiliza kwa makini.
“Njasi unasema kweli?!!! Anaishi wapi huyo bwana?”
Qeenlyn anamuuliza shoga yake huku akiwa na shauku yakutaka kumjua.
“Anaishi Tabata Segerea mwisho pale kituoni nimeelekezwa ninapajua hadi nyumba anayoishi, yaani aliniandaa hadi mwili wangu ulikuwa umemkubali. Kwani amenikojoza bwana yule zaidi ya mara tatu kwa mikono yake. Yule ni bingwa wa mambo ya ndani ya kuta 4. Ana Dhakari hiyo, siyo nyembamba, siyo nene. Siyo ndefu ya karaha.”
Njasi anamtangaza Dobe kwa Qeenlyn bila kutoa risiti.
“Ehee sasa kwani wewe umekutana nae wapi shosti?”
Qeenlyn anamsaili kwa makini huku ndani ya nafsi yake, anamtamani amuone na yeye afanyiwe mambo hayo, akojoe mikononi mwake.
“Shost weee, kule kwenye massage nilipokwenda kukandwa bibi wee, nikakutana na huyo kijana yaani uzalendo umenishinda. Kwanza mikono yake laini, pili anajoto jingi mwilini mwake, kiasi akikushika tu kwa mikono yake, lazima mwili wako usisimkwe.”
Njasi anamtangaza Dobe kwa gharama nafuu sana.
“Sasa shoga mtu akikufanyia massage ndiyo uuone uume wake, kwani mlikuwa uchi hamkuwa na nguo kabisa?!”
Qeenlyn alikuwa akimdadisi shoga yake, huku akiwa makini sana.
“Shost wee, nilikuwa nimevaa kama tunavyofanya massage kila ninapotaka kukanda mgongo na viungo vyangu, ila huyo bwana, alikuwa akinimassage hadi nikajikuta ninatoa nguo zangu, ili nile mzigo. Kwani nimelegea kila mahala, nyege zimepanda hadi nimekojoa mara tatu, lakini chini kukawa kunataka uume. Sasa na yeye maashaallah kama nilivyokueleza amejaaliwa.”
Njasi alivyofika hapo, Qeenlyn akaanza kusikia vitu vinamtembea mwilini mwake. Macho yake yakaanza kuwa mavivu, sauti yake ikaingiliwa na kikohozi, yaani nyege zilikuwa zimemtembelea ghafla.
“Ehee kwa hiyo na yeye akavua mkapiga show? Vipi anajua lakini huko kukaza kwenyewe, kwani kuna baadhi ya wanaume, ni mahodari wa kumuandaa mwanamke, ikifika wakati wa kukutanisha vinena, degedege linawaingia wanamwaga wala wewe hujausikilizia huo uume kwenye vyumba vyake saba! Wengi wanaishia chumba cha kwanza tu, akikukuruka sana, ataingia chumba cha pili anamaliza! Kwisha habari yake. Anakuiacha na nyege, akuumize na stress.”
Qeenlyn anaposema maneno hayo wakatungua kicheko kikubwa.
“Hehee, kantangazeee!!!”
Watu wa meza za jirani wakawatizama lakini wao wala hawana habari.
“Shost uongo dhambi sijagongana nae. Kwani wakati Yule bwana anataka kunifanya tu, tukafumwa na meneja wake. Ila mie nilikuwa hoi nimeshakojoa mfululizo vitatu, hadi nikaishiwa nguvu kabisa. Sasa nimekutafuta shost wangu wewe ninakuamini, ninataka twende sote hadi katika ile nyumba ili tukamuulizie afya yake na tumuone, mie nishakolea shoga yangu. Ila nina wasiwasi je akiwa na mke itakuwaje?”
Njasi anasema maneno hayo akawa katika tafakuri nzito.
“Sikiliza shost, tusiumize vichwa bure, mie ninafikiri tufanye hivi, nielekeze wasifu wake ulivyo, ili mie niende wewe usiingie kwani kama kweli ana mke, macho yenu yakionana tu kama na yeye kakolea mzigo huo, itakuwa rahisi mkewe kujua. Ila kwa kuwa mie hanijui hatotaharuki atakaponiona hivyo itakuwa rahisi kuzungumza nae na kukuletea mzigo wako, na kama akiwa yupo Single basi nitakuvuta kwa simu utakuja.”
Mipango hiyo wakaijadili kisha wakaiboresha wakapata jambo la kuingia nalo katika nyumba anayoishi. Na kwamba Njasi atakaa nje hatoingia ndani. Atakaa jirani tu.
Wakaingia katika gari ya Qeenlyn Toyota Vitz, wakaelekea Segerea mwisho, kwa maelekezo ya Njasi kama alivyoelekezwa na Meneja.
Gari ikaegeshwa mbali kama nyumba ya tatu kutoka nyumba anayoishi Dobe, Qeenlyn akashuka akaelekea katika nyumba hiyo. Alipofika akabisha hodi mlangoni, akasubiri. Mara baada ya muda mlango ulifunguliwa na Baby Mwanamtama.
Qeenlyn akakaribishwa ndani akashangaa kumuona mama mtu mzima amevaa Khanga moja, ana umbo zuri sana.
Akatupisha macho yake harakaharaka pale sebuleni, akaona vyombo na chakula chenye kunukia. Akili yake ikamuonesha kuwa Mama huyu alikuwa akila na mtu, kwani angelikuwa anakula peke yake, kusingekuwa na mataalazi ya Kawa, na sinia kubwa na ghasia anazoziona, bali ingekuwa sahani moja tu na kijiko chake, kuonesha mlaji ni mmoja ambae ni yeye.
“Karibu nikusaidie nini?”
Baby Mwanamtama anamuuliza mgeni wake huku anamtazama usoni mwake, wanja pambe umemkaa vyema, macho minal aal yamepamba uso wake jamali. Rangi yake ya asili na umbo lake pamoja na mavazi yake aliyovaa, na manukato ya mwilini mwake, yalimfanya Baby Mwanamtama, akae tayari tayari.
“Naitwa Qeenlyn George, ninashida na Dobe sijui nimemkuta? Kwani nina maagizo yake, nimepewa na Njasi ninataka kumpa.”
Baby Mwanamtama anamtazama Qeenlyn kutokea juu hadi chini, anamthaminisha vilivyo kisha anamwambia kwa mkato.
“Dobe amehama humu!”
Qeenlyn anashangaa sana.
“Mama sama…!”
“Koma kama ulivyokoma ziwa la mama yako! Usinizeeshe mie tafadhali eee? Mie na weye tumecheza mchezo mmoja, kisa chakuniita mie mama. Dobe amehama hakai humu, na ameondoka na deni langu la kodi ya miezi mitatu, umekuja nayo umlipie?”
Qeenlyn anashangaa sana kufananishwa umri wake na wa mama mtu mzima! Akaona hakuna maelewano, akainuka akapangusa nguo yake kwenye makalio akaondoka, akapeleka kwa Njasi majibu na mazingira aliyokutana nayo.
Wakakaa kwenye gari wakajadili kwa muda, ikawathibitikia kuwa Dobe yumo ndani na bila shaka mama hadi anakuwa mkali kwake, itakuwa anakula mzigo na kijana!
Wakafikiri sana, Njasi machozi yanamtoka kwa wivu na uchungu mkubwa kwa maelezo aliyoambiwa na shoga yake, hatimae akakata shauri.

***
“Baby, halow, Halow baby?”
Ninaita huku wasiwasi ukiwa umeniingia sana. Ninakwenda sebuleni macho yangu yanapata makengeza ya mwaka kwa ninachokiona!!

11
Nikiwa nimesimama wima sebuleni, siamini macho yangu, ninamuona Baby Mwanamtama, amekaa katika kiti cha kulia cha watu wawili, Meneja amekaa katika kiti cha kati cha mtu mmoja, na Njasi amekaa katika kiti cha kushoto cha watu watatu, wote kwa pamoja wameacha kuzungumza wananitazama usoni.
Kiasi ninafadhaika sana. Kwani nilipo nimevaa upande mmoja tu wa Khanga ya Baby Mwanamtama. Sikutarajia kama asubuhi hii nitakutana na Njasi na meneja kwa pamoja katika hali hii.
“Wewe uliesema Dobe amehama hapa, huyu ni nani?”
Njasi anamuuliza Baby Mwanamtama huku akimtazama usoni kwa hasira, ameukunja uso wake.
“Usinite wewe mimi umesikia? Niite Baby Girl kama ukipenda, na ikiwa hutaki roho yako ina mfundo basi niite Mrs Dobe wa ukweli upo?!”
Baby Mwanamtama anamwambia hivyo Njasi, na anajishebedua mashauzi ya karne!
Lakini ninapomtazama Njasi kwa majibu aliyojibiwa, ninamuona anamnyali kwa sana yaani anamshusha na kumpandisha. Macho yake makubwa na mdomo unavyofanywa kama kuku ndiyo angetizamwa hivyo, basi kuku huyo asingelikunywa maji angeliondoka!
Ninamtazama meneja wangu, ninamuona ananitazama kwa chuki na hasira, akiwa katika mikausho mikali kabisa.
“Jamani hamjambo?”
Mie ninawasalimia ili nijue kulikoni na kwa namna gani hadi wamekuwa watu hawa mahala hapa.
“Jambo likupate wewe siye tukuombee!!!”
Meneja ananijibu kwa jeuri, ninamshangaa simmalizi!
“Mbona siwaelewi jamani kwani kuna nini maana naona shari nje nje imekuwaje?!”
Ninawauliza Meneja na Njasi, lakini wao wala hawana habari yakunijuza kinyume chake wananitazama kama mtu niliepotea vile.
“Dobe Boy, njoo Baby. Njoo ukae nami honey wangu, usisimame wima ukatunyonya damu bure ukaja kupata damu za vizushi, kwani hawa watu siwaelewi mie kabisa naona wananiletea fushi tu hapa, asubuhi asubuhi kuharibiana siku tu, na kutiana mikosi ya bure.”
Baby Mwanamtama ananambia maneno hayo huku akinitazama na mie ninamtazama meneja ninamuona ananitolea macho kama yakunikataza kukaa nae.
Ninamtazama Njasi, ninamuona anatikisa kichwa chake kwa masikitiko!
Nami ninaamua bila woga ninasogea kwa Baby Mwanamtama katika kiti cha watu wawili alichokaa, ninakaa pembeni na Khanga yangu kiunoni.
Baby anainua miguu yake ananiwekea juu ya mapaja yangu.
“Dobe umekumbwa na nini lakini yaani ndiyo umekuwa hivyo?!”
Meneja ananitupia swali mara tu ninapokaa kitako na Baby kuniwekea miguu yake.
“Bosi mbona nipo sawa tu kwani vipi?”
Ninamuuliza Meneja wangu huku ninamtizama usoni moja kwa moja.
“Haupo sawa Dobe, haupo sawa nakataa! Haya kwa sababu gani zilizokusibu hadi umezima simu yako, ninakutafuta sikupati kwenye simu tangu jana?! Sasa ile nyumba uliyoniagiza nikutafutie nimeshaipata na nimeshamalizana nao wenyewe nimekufata hapa ili ukahamie tu.”
Meneja wangu maneno yake ayasemayo, naona ameamua aniharibie.
Ninamtazama usoni Meneja wangu, ninagundua kuwa ameshikwa na wivu uliopitiliza.
“Hehee Kantangazee!!! Haami mtu hapa bibiee upo?! Dobe hapa keshafika, na kwa taarifa yako Dobe Boy kwa sasa ndiyo Baba mwenye nyumba hii, na yeye ndiyo msimamizi wa kila kilicho changu. Hatoki wala kufanya jambo ila kwa idhini yangu. Kama umempangia chumba katafute mtu wa kwenda kulala nae, lakini Dobe hapa haami hata kwa mtutu wa Bunduki! Labda mie sijawekwa mkoleni kufundwa, lakini kama nilifundwa nikiwa uchi ndani, sina hata ulepe wa Khanga, Dobe hapa hatoki na wewe huna wala huijui mizungu yakumtoa. Usitafute nikakutangaza bure!”
Baby Mwanamtama anamwambia meneja wangu kwa kejeli na kedi ya hali ya juu.
“Usimjibie mwenyewe anao mdomo, mwache ajibu mwenyewe. Dobe unataka kuhama hapa au hutaki?!”
Meneja ananiuliza huku ananitazama usoni.
“Baby nikune mgongoni kuna kipele kinaniwasha, hapo karibu na kiuno.”
Mwanamtama anayakhanithi maneno yenyewe, kisha anailegeza Khanga yake anayaachia matiti yake ya duara yanaonekana.

HAYA TUNAZIDI KUSONGA MBELE. ITAENDELEA 





Ludewa yetu na maendeleo yetu posted by barnabas njenjema, kutoka Ludewa
Share on Google Plus

About Rafiki Fm Ludewa

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: