Saturday, April 2, 2016

Umeme sasa bei chee...Soma mchanganuo hapa..!




MATUMIZI YA NYUMBANI:
Watalipa Sh100 kwa uniti moja wengine watalipa Sh292 badala ya Sh298 kutegemea matumizi. Malipo ya huduma ‘service charge’ ya 5,520 kila mwezi yameondolewa.

VIWANDA VYA KATI:
Watalipia Sh195 kwa uniti kutoka Sh200 ya sasa huku wakiendelea kutozwa ‘service charge’ ya Sh14,233.

NGUZO ZA UMEME:
Mteja asiyehitaji nguzo atalipa Sh272,000 kwa waliopo mjini na Sh150,000 kwa vijijini. Wanaohitaji nguzo moja watalipia Sh436,964 kwa mjini na Sh286,220 kwa vijijini.

BIASHARA NA VIWANDA:
Walikuwa wanatozwa Sh298 kwa uniti na sasa watatakiwa kulipa Sh292, huku wakiondolewa ‘service charge’ ya Sh6,000 kila mwezi.

KAMPUNI ZA MADINI:
Watatakiwa kulipia Sh152 kwa kila uniti moja, ikiwa ni punguzo la Sh6. Hii ni pamoja na Shirika la Umeme Z’bar (Zeco).

UMEME NJIA TATU:
Watakaounganishwa kwenye njia tatu; ndani ya mita 30 watalipia Sh772,893 wakati wale wa ndani ya mita 70 watapaswa kulipa Sh1,058,801 huku ndani ya mita 120 wakilipia Sh1,389,115.



Ludewa yetu na maendeleo yetu

No comments:

Post a Comment