Sunday, January 18, 2015

WEMA SEPETU ALIA MIMBA YA KANUMBA

MWANADADA asiyeishiwa habari, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ anadaiwa kujutia mimba yake aliyopachikwa na aliyekuwa staa mkubwa wa sinema za Kibongo, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ wakati wa mapenzi yao.
Chanzo makini kilicho karibu na Wema kilieleza kwamba, mwanadada huyo kwa sasa yupo kwenye wakati mgumu huku akijutia mimba aliyopewa na Kanumba ambayo ilichoropoka kwa bahati mbaya na huyo ndiye mwanaume pekee aliyewahi kumpa ujauzito.

No comments:

Post a Comment