Habari mbali mbali za kitaifa;kimataifa;michezo na burudani; tunakuhabarisha kutoka ludewa mkoa wa Njombe na wilaya ya Ludewa
Thursday, December 4, 2014
Matokeo ya mechi za Ligi kuu ya England
Ligi kuu ya England imeendelea usiku huu kwa michezo mine iliyozikutanisha timu nane za ligi hiyo .
Kwenye uwanja wa Emirates , Arsenal waliweza kushinda mchezo wao wa pili mfululizo baada ya kuwafunga Southampton 1-0 ukiwa ni ushindi wao wa pili mfululizo wakishinda kwa bao moja .
Bao hilo lililowapa Arsenal ushindi lilifungwa na Alexis Sanchez ukiwa ushindi wa kwanza kwa Arsenal dhidi ya timu iliyoko kwenye nafasi za tatu bora .
Alexis Sanchez ameifungia Arsenal mabao 8 kwenye EPL msimu huu.
Kwingineko Chelsea walishinda mchezo wao dhidi ya Tottenham kwa matokeo ya 3-0 . Ushindi huo ulikuja baada ya mabao ya Edin Hazard , Didier Drogba na Loic Remy .
Edin Hazard akifunga bao la kwanza kwa chelsea.
Mshambuliaji Didier Drogba akifunga bao la pili kwenye mchezo dhidi ya Tottenham.
Katika mchezo mwingine Hull City na Everton walitoka sare ya 1-1 , na Man city wakawafunga Sunderland 1-4 .
Matokeo haya yanamaanisha kuwa Chelsea wanaendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 33 wakiwa wamewazidi Man city kwa pointi sita , Southampton ambao leo hii wamepoteza mchezo wao wa pili mfululizo wamejikuta wakishuka zaidi huku tofauti yao na Man United inayoshika nafasi ya 4 ikiwa pointi moja pekee .
No comments:
Post a Comment